{"id":1866,"date":"2022-03-04T23:38:01","date_gmt":"2022-03-05T03:38:01","guid":{"rendered":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/?p=1866"},"modified":"2022-03-05T01:38:21","modified_gmt":"2022-03-05T05:38:21","slug":"kutoka-1-usomaji-wa-biblia","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1866","title":{"rendered":"Kutoka 1: Usomaji wa Biblia"},"content":{"rendered":"<p><strong>Kutoka 1:<\/strong><\/p>\n<p><strong>\u00a0<\/strong><\/p>\n<hr \/>\n<p><span style=\"color: #003366;\"><strong><em>1 <\/em><\/strong>Basi majina ya wana wa Israeli walioingia Misri ni haya; kila mtu pamoja na jamaa zake walikuja pamoja na Yakobo.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>2\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>3\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>4\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>5\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>6\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Yusufu akafa, na ndugu zake wote, na watu wote wa kizazi kile.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>7\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>8\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>9\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>10\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>11\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>12\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>13\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>14\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>15\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>16\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>17\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>18\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Basi mfalme wa Misri akawaita wale wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto waume wawe hai?<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>19\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>20\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Basi Mungu akawatendea mema wale wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>21\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>22\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha huyo Farao akawaagiza watu wake, akisema, Kila mtoto mwanamume atakayezaliwa mtamtupa mtoni, na kila mtoto mwanamke mtamhifadhi hai.<\/span><\/p>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<h3>2-BSG-1D: MDOKEZO WA SURA.<\/h3>\n<p><em>Mwongozo wa Kujifunza Biblia\/ <strong>Muhtasari wa Sura<\/strong>\/ Kutoka 1, (2-BSG-1D)\/ <\/em><strong><em>Dhima<\/em><\/strong><em>: Israeli Yateswa Huko Misri.<\/em><\/p>\n<hr \/>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Kifupi:<\/strong> <\/span>Majina ya wana wa Yakobo walioingia Misri (1-5); kifo cha kizazi hicho (6); ongezeko kubwa la uzao wao (7); majaribio yasiyo na mafanikio ya mfalme mpya wa Misri ili kuzuia ukuaji wa Israeli (8-14); amri katili za mfalme kwa wakunga (15-21); amri ya mfalme kuwaangamiza watoto Waebrania wote wachanga wa kiume (22).<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Wahusika<\/strong>:<\/span> Mungu (Asiyeonekana), Yusufu, wana 12 wa Israeli, Farao, Shira, Pua.<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Andiko Kuu<\/strong>:<\/span> \u201cBasi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu. Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi. Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.\u201d (Kutoka 1:8\u201310)<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Neno Kuu<\/strong>:<\/span> Hali ngumu ya Utumwa (fasili ya 14).<\/p>\n<p><strong><span style=\"color: #993300;\">Virai Teule<\/span> <\/strong>\u2014 Yusufu akafa; ni wengi na wana nguvu kuliko sisi; Njooni, tuwatendee kwa werevu; Katika chokaa na matofali; wakunga wa Kiebrania; Lakini wakunga hao walimcha Mungu; \u201cKwa nini mmefanya jambo hili? Mungu akawatendea mema wakunga hao; Atatupwa mtoni.<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Maandiko Makini: <\/strong><\/span>Kutoka 1:1-4, 5, 6, 7, 8, 9-10, 11, 12, 15-16, 17, 18, 19, 20-21, 22.<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Mgawanyo wa Mawazo Makuu<\/strong><\/span> \u2014 wana 12 wa Yakobo walioingia Misri (1\u20136); Sababu za Mateso (7\u201310); Matokeo ya Mateso (Kut. 1:11\u201322)<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Matukio ya Biblia: <\/strong><\/span>[<span style=\"color: #0000ff;\">Matukio yanayofanyika<\/span>]\u2014<\/p>\n<ol>\n<li>Waisraeli wanakuwa watumwa huko Misri Kut. 1:8\u201314<\/li>\n<li>Utumwa huko Misri Kut. 1:8\u201312:32<\/li>\n<li>Kutoka Misri Kut. 1:8\u2013Kumb 34:8<\/li>\n<li>Farao anawaambia wakunga wawaue watoto Waebrania wa kiume Kut. 1:15\u201319<\/li>\n<li>Watoto wa kiume wanauawa huko Misri Kut. 1:15\u201322<\/li>\n<li>Maisha ya awali ya Musa Kut. 1:15\u20132:24<\/li>\n<li>Mungu huwapa wakunga familia Kut. 1:20\u201321<\/li>\n<li>Farao anawaambia Wamisri kutupa watoto wa kiume ndani ya Naili Kut. 1:22<\/li>\n<\/ol>\n<p>[<span style=\"color: #0000ff;\">Matukio Yaliyotajwa<\/span>] \u2014<\/p>\n<ol>\n<li>Yakobo anaenda Misri \u2022 Mwa. 46:5\u20137 (Kut. 1:5)<\/li>\n<li>Yusufu anakufa \u2022 Mwa. 50:22\u201326 (Kut. 1:6)<\/li>\n<\/ol>\n<p><strong><span style=\"color: #993300;\">Mdokezo wa Mambo Muhimu<\/span> <\/strong>\u2014<\/p>\n<ol>\n<li>Agano la Ibrahimu (Mwa. 12:1-3; 13:15; 15:18-21; 17:1-6)<\/li>\n<li>Unabii uliotimia wa 15:13-16 vs. miaka 400 ya mateso.<\/li>\n<li>Ukombozi: Musa, mtangulizi wa Yesu Kristo.<\/li>\n<li>Majaribu: Jinsi ya kukabili dhuluma, dhiki, utumwa.<\/li>\n<li>Utii: Kuchukua hatua pale sheria za nchi zinapopingana na Sheria ya Mungu.<\/li>\n<li>Uaminifu wa Mungu katika kutimiza Ahadi Zake: Kuzaliwa kwa Musa (Kut. 2:1-10)<\/li>\n<li>Huruma ya Mungu: Watoto Wake wanapoomba msaada, Yeye husikia na kuguswa na mateso yao! (Kut. 2:23-25)<\/li>\n<\/ol>\n<p><strong><span style=\"color: #993300;\">Uchunguzi wa Muktadha Msingi<\/span> <\/strong>\u2014Wafalme wa Misri.<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Mambo ya Kujifunza Zaidi <\/strong><\/span>\u2014 Matarajio ya AK ya kanisa; Jinsi gani miaka 400 ya Mwa. 15:13-16 inahusiana na miaka 430 ya Kut. 12:40-41 na Gal. 3:16-17?<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Wazo Makini<\/strong>:<\/span> Daima kuna pambano (vita) kati ya uzao wa mwanamke na uzao wa nyoka (Mwa. 3:15). Mungu alikuwa akitekeleza mpango Wake wa ukombozi kupitia watu Wake Israeli, yaani, kuzaliwa kwa Masihi. Wakati huohuo, Shetani (kupitia mfalme mpagani) alijaribu kuzuia makusudi ya Mungu kwa kulifuta taifa lililochaguliwa. Mara tatu katika sura hiyo, Farao ameamua kuwaangamiza Waebrania (Kut. 1:7-10, 15-16, 22), lakini Mungu anaingilia kati! Mungu alimwinua Musa ili kuleta ukombozi mkubwa kwa Israeli kwa wakati ulioteuliwa. Katika wakati ulioteuliwa, Kristo alizaliwa (Gal 4:4). Katika wakati ulioteuliwa, Kristo atatokea tena! \u201cAtakuja tena, <u>siyo kushughulikia dhambi zetu<\/u>, bali kuwaletea <u>wokovu wote wamngojeao kwa shauku<\/u>.\u201d (Waebrania 9:28, NLT). Watu wa Mungu watajaribiwa (Mat 5:10; 2 Tim 3:12; Ufu. 2:10), lakini katika mateso yao, atawategemeza wote wanaomtumaini.<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\"><strong>Neno la Faraja<\/strong>:<\/span> \u201cNaam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo Lako na fimbo Yako vyanifariji.\u201d (Zaburi 23:4)<\/p>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<div class='share-to-whatsapp-wrapper'><div class='share-on-whsp'>Share on: <\/div><a data-text='Kutoka 1: Usomaji wa Biblia' data-link='https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1866' class='whatsapp-button whatsapp-share'>WhatsApp<\/a><div class='clear '><\/div><\/div>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Kutoka 1: \u00a0 1 Basi majina ya wana wa Israeli walioingia Misri ni haya; kila mtu pamoja na jamaa zake walikuja pamoja na Yakobo. 2\u00a0Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda; 3\u00a0na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini; 4\u00a0na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri. 5\u00a0Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni <a class=\"read-more-link\" href=\"https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1866\"><br \/>&#8230;read more<\/a><\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":1561,"comment_status":"closed","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"om_disable_all_campaigns":false,"_monsterinsights_skip_tracking":false,"_monsterinsights_sitenote_active":false,"_monsterinsights_sitenote_note":"","_monsterinsights_sitenote_category":0,"footnotes":""},"categories":[23],"tags":[],"class_list":["post-1866","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-usomaji-vidokezo"],"jetpack_featured_media_url":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-content\/uploads\/2020\/10\/Default-Featured-Image-2020.jpg","_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1866","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=1866"}],"version-history":[{"count":2,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1866\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":1868,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1866\/revisions\/1868"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/media\/1561"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=1866"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=1866"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=1866"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}