{"id":1939,"date":"2022-08-10T07:47:31","date_gmt":"2022-08-10T11:47:31","guid":{"rendered":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/?p=1939"},"modified":"2022-08-21T06:58:50","modified_gmt":"2022-08-21T10:58:50","slug":"waamuzi-1-mdokezo-wa-sura","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1939","title":{"rendered":"Waamuzi 1: Usomaji, Vidokezo"},"content":{"rendered":"<p><span style=\"color: #ff0000;\">WAAMUZI 1D: MDOKEZO WA SURA.\u00a0<\/span><\/p>\n<p><em>Mwongozo wa Kujifunza Biblia\/ <strong>Muhtasari wa Sura<\/strong>\/ Waamuzi 1, (7-BSG-1D)\/ <\/em><strong><em>Dhima<\/em><\/strong><em>: Kushindwa kwa Israeli Kuwafukuza Wakanaani Wote katika Nchi ya ahadi.<\/em><\/p>\n<hr \/>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Wahusika<\/strong>:<\/span> Mungu, Yuda, Simeoni, Adoni-bezeki, Kalebu, Aksa, Othnieli.<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Andiko Kuu<\/strong>:<\/span> \u201cSasa baada ya Yoshua kufa ikatokea kwamba wana wa Israeli walimuuliza BWANA, wakisema, \u2018Nani atakayekwea kwanza kwa ajili yetu dhidi ya Wakanaani ili kupigana nao?\u2019 Naye BWANA akasema, \u2018Yuda atakwea. Hakika, nimeitia nchi hiyo mkononi mwake.\u2019\u201d (Waamuzi 1:1\u20132)<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Neno Kuu<\/strong>:<\/span> Kumuuliza BWANA \u2013 Amu. 1:1; 20:23, 27; 1 Sam 22:10; 23:2, 4; 28:6; 30:8; 2 Sam 2:1; 5:19, 23 (Ni mara ngapi kirai hiki kinapatikana katika maisha yangu?)<\/p>\n<p><strong><span style=\"color: #0000ff;\">Virai Teule<\/span> <\/strong>\u2014 \u201chawakuwafukuza\u201d \u2013 (Yuda, Manase, Efraimu, Zabuloni, Asheri, Naftali, na Dani)<\/p>\n<p><strong><span style=\"color: #0000ff;\">Maandiko Makini:<\/span> <\/strong>Ushindi nusu &amp; usio kamili (angalia Waamuzi 1:19, 21, 27, 29, 30, 31, 33, 34)<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Matukio ya Biblia: <\/strong><\/span>[Matukio Yanayofanyika]\u2014<\/p>\n<ol>\n<li>Yuda na Simeoni wamshinda Adoni-bezeki (3\u20137)<\/li>\n<li>Yuda yaivamia Yerusalemu (8)<\/li>\n<li>Wakeni wanakaa Yuda (16)<\/li>\n<li>Simeoni na Yuda waiteka Sefathi (17)<\/li>\n<li>Yuda aiteka Gaza, Ashkeloni, na Ekroni (18)<\/li>\n<li>Benjamini ashindwa kuwafukuza Wayebusi (21)<\/li>\n<li>Waisraeli washindwa kuteka maeneo kadhaa (21\u20132:5)<\/li>\n<li>Makabila ya Yusufu yaishinda Betheli (22\u201326)<\/li>\n<li>Manase ashindwa kuwafukuza Wakanaani (27\u201328)<\/li>\n<li>Efraimu ashindwa kuwafukuza Wakanaani (29)<\/li>\n<li>Zabuloni ashindwa kuwafukuza Wakanaani (30)<\/li>\n<li>Asheri ashindwa kuwafukuza Wakanaani (31\u201332)<\/li>\n<li>Naftali ashindwa kuwafukuza Wakanaani (33)<\/li>\n<li>Dani ashindwa kuwafukuza Waamori (34\u201336)<\/li>\n<\/ol>\n<p>[Matukio Yaliyotajwa]<\/p>\n<ol>\n<li>Waisraeli waiteka Lakishi \u2022 Yos 10:31\u201333 (Amu. 1:9)<\/li>\n<li>Waisraeli waiteka Libna \u2022 Yos 10:29\u201330 (Amu. 1:9)<\/li>\n<li>Waisraeli waiteka Debiri \u2022 Yos 15:15\u201317 (Amu. 1:9, 11\u201313)<\/li>\n<li>Waisraeli waiteka Egloni \u2022 Yos 10:34\u201335 (Amu. 1:9)<\/li>\n<li>Waisraeli waiteka Hebroni \u2022 Yos 15:14 (Amu. 1:9\u201310, 20)<\/li>\n<li>Kalebu ampa Aksa chemchemi \u2022 Yos 15:18\u201319 (Amu. 1:14\u201315)<\/li>\n<li>Musa afanya maombezi, na Mungu aahidi hukumu \u2022 Hes. 14:13\u201338 (Amu. 1:20)<\/li>\n<\/ol>\n<p><strong><span style=\"color: #0000ff;\">Mdokezo wa Mambo Muhimu<\/span> <\/strong>\u2014 Yuda &amp; Simeoni: Mfululizo wa kwanza wa Ushindi (1:1\u201319); Yuda: Ishara ya kwanza ya kushindwa (1:19\u201321); Ushindi usio kamili (1:22\u201336); Kazi ya Shokoa (1:30, 33, 35).<\/p>\n<p><strong><span style=\"color: #0000ff;\">Uchunguzi wa Muktadha Msingi<\/span> <\/strong>\u2014 Ugawaji wa Ardhi; Kupanga Ndoa; Vita -(kunyang&#8217;anywa ardhi); Zawadi &#8211; (kutoa kama malipo au urejeshaji); Utumwa &#8211; (utumikishwaji wa shokoa); Upelelezi &#8211; (ujasusi, na kukusanya taarifa za upelelezi); Magari &#8211; Vitu visivyo hai vinavyotumiwa kwa usafiri: &#8220;magari ya chuma\u201d (Amu. 1:19)<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Mambo ya Kujifunza Zaidi <\/strong><\/span>\u2014 Utangulizi kwa Waamuzi; Wazao wa Anaki (Sheshai, Ahimani, na Talmai, Amu. 1:10).<\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><strong>Wazo Muhimu<\/strong>:<\/span> Kushindwa kwa Israeli kuteka Kanaani kwa sababu ya dhambi yao (1:1-36). \u201cWaamuzi huanzia pale ambapo Yoshua aliishia, yaani, nchi ya ahadi ikiwa imeshinda vitani, lakini haijakaa kabisa au kutekwa kikamilifu. Kwa kweli, wapagani wengi katika nchi hii, wakazi Wakanaani bado wangalipo. Sura ya kwanza inabainisha muhtasari wa majaribio ya watu wa Mungu kutii agizo la kuwaondoa watu na ushawishi wa kidini wa Kanaani kutoka katika nchi waliyogawiwa. Nusu ya kwanza ya sura (1:1\u201320) inarejelea mafanikio ya Yuda na Simeoni katika jitihada hii. Sehemu iliyosalia ya sura (1:21\u201336) inaelezea kuzidi kushindwa kwa jitihada za makabila mengine kufanya vivyo hivyo. Hatimaye, wanafanyia maridhiano mabaya utelekevu wao pekee kwa BWANA. Kwa sababu ya kushindwa kwa watu wa Mungu kufuata maagizo Yake, katika sura inayofuata <u>atajibu kwa kuwakabili<\/u> kupitia mjumbe wa kiungu na kujaribu uaminifu wao kwa nchi hiyo kukaliwa na mfululizo na watesi wa aina mbalimbali.\u201d \u2013[Douglas Mangum, Ed., Lexham Context Commentary: Old Testament, Lexham Context Commentary, (Bellingham, WA: Lexham Press, 2020), Jdg 1:1\u201336].<\/p>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<p><span style=\"color: #ff0000;\">WAAMUZI 1C: SURA YA LEO<\/span><\/p>\n<p><strong><em><span style=\"color: #0000ff;\">Usomaji wa Biblia kwa Mpango<\/span>\/<\/em><\/strong><em> Kitabu cha Waamuzi 1, (7-BSG-1C)\/<span style=\"color: #0000ff;\"> <strong>Dhima<\/strong>:<\/span><\/em><em> Kushindwa kwa Israeli Kuwafukuza Wakanaani Wote katika Nchi ya ahadi.<\/em><\/p>\n<hr \/>\n<p>&nbsp;<\/p>\n<p>WAAMUZI 1:<\/p>\n<p><span style=\"color: #003366;\">1 Ikawa baada ya kufa kwake Yoshua, wana wa Israeli wakamwuliza Bwana, wakisema, Ni nani atakayekwea kwanza kwa ajili yetu juu ya Wakanaani, ili kupigana nao?<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>2\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Bwana akasema, Yuda atakwea; tazama, nimeitia hiyo nchi mkononi mwake.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>3\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Ndipo Yuda akamwambia Simeoni ndugu yake, Kwea wewe pamoja nami katika kura yangu, ili tupate kupigana na Wakanaani; kisha mimi nami nitakwenda pamoja nawe katika kura yako. Basi Simeoni akaenda pamoja naye.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>4\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Yuda akakwea; naye Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mkononi mwao; nao wakawapiga huko Bezeki watu elfu kumi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>5\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Wakampata huyo Adoni-bezeki huko Bezeki; wakapigana naye, nao wakawapiga Wakanaani na Waperizi.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>6\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Lakini Adoni-bezeki akakimbia; nao wakamwandamia na kumshika, wakamkata vyanda vyake vya gumba vya mikono na vya miguu.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>7\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Adoni-bezeki akasema, Wafalme sabini, waliokuwa wamekatwa vyanda vyao vya gumba vya mikono na vya miguu, waliokota chakula chao chini ya meza yangu; kama nilivyofanya mimi, Mungu amenilipa vivyo. Wakamleta Yerusalemu naye akafa kuko.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>8\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha wana wa Yuda wakapigana na Yerusalemu, wakautwaa, wakaupiga kwa makali ya upanga, na kuupiga moto huo mji.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>9\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Baadaye wana wa Yuda wakatelemka ili wapigane na hao Wakanaani waliokaa katika nchi ya milimani, na nchi ya Negebu, na nchi ya Shefela.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>10\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha Yuda akawafuatia hao Wakanaani waliokaa katika Hebroni; (jina la Hebroni hapo kwanza ulikuwa ukiitwa Kiriath-arba;) nao wakamwua Sheshai, na Ahimani, na Talmai.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>11\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha kutoka hapo akawafuatia wale wenye kukaa Debiri. (Jina la Debiri hapo kwanza ulikuwa ukiitwa Kiriath-seferi.)<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>12\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Huyo Kalebu alisema, Yeye atakayeupiga Kiriath-seferi na kuutwaa, nitamwoza mwanangu Aksa awe mkewe.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>13\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Naye Othnieli, mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, aliutwaa; basi akamwoza mwanawe Aksa.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>14\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Ikawa hapo alipokwenda kukaa naye, huyo mwanamke akamtaka ili aombe shamba kwa baba yake; na huyo mwanamke akashuka katika punda wake; Kalebu akamwuliza, Una haja gani utakayo?<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>15\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Mwanamke akasema, Nipe baraka; kwa kuwa wewe umeniweka katika nchi ya Negebu, basi unipe na vijito vya maji pia. Kalebu akampa vile vijito vya maji vya juu na vijito vya chini.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>16\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Hao wana wa Mkeni, huyo shemeji yake Musa, wakakwea juu kutoka katika huo mji wa mitende, pamoja na wana wa Yuda, na kuingia hiyo nyika ya Yuda, iliyo upande wa kusini wa Aradi; nao wakaenda na kukaa pamoja na watu hao.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>17\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha Yuda akaenda pamoja na nduguye Simeoni, na wakawapiga Wakanaani waliokaa katika Sefathi, na kuuharibu mji kabisa. Na jina la mji huo ulikuwa ukiitwa Horma.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>18\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Pamoja na haya Yuda aliutwaa Gaza pamoja na mipaka yake, na Ashkeloni na mipaka yake, na Ekroni na mipaka yake.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>19\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Bwana alikuwa pamoja na Yuda; naye akawafukuza watu waliokaa katika nchi ya milimani; asiweze kuwafukuza hao waliokaa katika hilo bonde, kwa kuwa wao walikuwa na magari ya chuma.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>20\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha wakampa huyo Kalebu Hebroni, kama alivyonena Musa naye akawafukuza wale wana watatu wa Anaki.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>21\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Lakini wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa mji wa Yerusalemu; bali Wayebusi walikaa pamoja na wana wa Benyamini ndani ya Yerusalemu hata hivi leo.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>22\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Nyumba ya Yusufu nayo, wao nao walikwea kwenda juu ya Betheli; naye Bwana alikuwa pamoja nao.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>23\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha mbari ya Yusufu wakatuma watu waende kuupeleleza Betheli. (Jina la mji huo hapo kwanza ulikuwa ukiitwa Luzu.)<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>24\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Hao wapelelezi walimwona mtu atoka katika huo mji, wakamwambia, Tafadhali, utuonyeshe maingilio ya mji huu, nasi tutakutendea mema.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>25\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Basi akawaonyesha maingilio ya mji, nao wakaupiga huo mji kwa makali ya upanga; lakini huyo mtu walimwacha aende zake, na watu wote wa jamaa yake.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>26\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Huyo mtu akaenda katika nchi ya Wahiti, akajenga mji, akaliita jina la huo mji Luzu; nalo ndilo jina lake hata hivi leo.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>27\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Tena Manase hakuwatoa wenyeji wa Bethsheani na miji yake, wala hao waliokaa Taanaki na miji yake, wala hao waliokaa Dori na miji yake, wala hao waliokaa Ibleamu na miji yake, wala hao waliokaa Megido na miji yake; lakini hao Wakanaani walikuwa hawakukubali kuiacha nchi hiyo.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>28\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha ikawa, hapo Israeli walipokuwa wamepata nguvu, ndipo walipowatia hao Wakanaani katika kazi ya shokoa, wala hawakuwafukuza kabisa.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>29\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Efraimu naye hakuwatoa Wakanaani waliokuwa wakikaa katika Gezeri; lakini Wakanaani walikaa ndani ya Gezeri kati yao.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>30\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Zabuloni naye hakuwatoa wenyeji wa Kitroni, wala hao waliokaa katika Nahalali; lakini Wakanaani walikaa kati yao, wakalazimishwa shokoa.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>31\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Asheri naye hakuwatoa wenyeji wa Aka, wala hao waliokaa Sidoni, wala hao wa Alabu, wala hao wa Akzibu, wala hao wa Helba, wala hao wa Afeka, wala hao wa Rehobu;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>32\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>lakini Waasheri wakakaa kati ya Wakanaani, hao wenyeji wa nchi; kwa kuwa hawakuwafukuza.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>33\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Naftali naye hakuwatoa wenyeji wa Bethshemeshi, wala hao waliokaa Bethanathi; lakini alikaa kati ya Wakanaani, hao wenyeji wa nchi; pamoja na haya hao wenyeji wa Bethshemeshi, na wenyeji wa Bethanathi, wakawatumikia kazi ya shokoa.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>34\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Kisha Waamori waliwasukumiza wana wa Dani waende milimani; kwani hawakuwakubali kutelemkia bondeni;<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>35\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>lakini hao Waamori waliendelea kukaa katika kilima cha Heresi, na katika Aiyaloni, na katika Shaalbimu; pamoja na haya mkono wa hiyo nyumba ya Yusufu ulishinda, hata wakawalazimisha shokoa.<\/span><br \/>\n<span style=\"color: #003366;\"> <strong><em><sup>36\u00a0<\/sup><\/em><\/strong>Mpaka wa Waamori ulikuwa tangu huko kupandia Akrabimu, tangu hilo jabali, na juu yake.<\/span><\/p>\n<div class='share-to-whatsapp-wrapper'><div class='share-on-whsp'>Share on: <\/div><a data-text='Waamuzi 1: Usomaji, Vidokezo' data-link='https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1939' class='whatsapp-button whatsapp-share'>WhatsApp<\/a><div class='clear '><\/div><\/div>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>WAAMUZI 1D: MDOKEZO WA SURA.\u00a0 Mwongozo wa Kujifunza Biblia\/ Muhtasari wa Sura\/ Waamuzi 1, (7-BSG-1D)\/ Dhima: Kushindwa kwa Israeli Kuwafukuza Wakanaani Wote katika Nchi ya ahadi. &nbsp; Wahusika: Mungu, Yuda, Simeoni, Adoni-bezeki, Kalebu, Aksa, Othnieli. Andiko Kuu: \u201cSasa baada ya Yoshua kufa ikatokea kwamba wana wa Israeli walimuuliza BWANA, wakisema, \u2018Nani atakayekwea kwanza kwa ajili <a class=\"read-more-link\" href=\"https:\/\/tgvs.org\/injili\/archives\/1939\"><br \/>&#8230;read more<\/a><\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":1561,"comment_status":"closed","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"om_disable_all_campaigns":false,"_monsterinsights_skip_tracking":false,"_monsterinsights_sitenote_active":false,"_monsterinsights_sitenote_note":"","_monsterinsights_sitenote_category":0,"footnotes":""},"categories":[23],"tags":[],"class_list":["post-1939","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-usomaji-vidokezo"],"jetpack_featured_media_url":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-content\/uploads\/2020\/10\/Default-Featured-Image-2020.jpg","_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1939","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=1939"}],"version-history":[{"count":2,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1939\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":1948,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/1939\/revisions\/1948"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/media\/1561"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=1939"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=1939"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tgvs.org\/injili\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=1939"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}