Mti wa ujuzi wa Mema na Mabaya

February 5, 2022 in Mwongozo wa Maombi by TGVS

Mwanzo 2: Mwongozo wa Maombi/ 1-BSG-2B (Mwanzo 2:1-25)/ Dhima: Mti wa ujuzi wa Mema na Mabaya/ Wimbo:


 

Andiko Msingi: “Na BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula; lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” (Mwanzo 2:16–17)

Maelezo ya Ufunguzi: Dhima kuu tatu zinajitokeza katika sura hii: Sabato, Ndoa na Uhuru wa Kuchagua (kama inavyowasilishwa na Mti wa ujuzi wa mema na mabaya). Ilikuwepo miti mingi katika bustani, lakini miwili ni muhimu sana: Mti wa Uzima ambao unatokea mara kadhaa katika Maandiko (Mit. 3:18; 11:30; 13:12; 15:4; Ufu. 2:7; 22:1–2, 14, 19); na Mti wa ujuzi wa mema na mabaya, ambao umetajwa hapa tu (Mwa. 2–3). “Uwepo tu wa mti huu katika bustani kulionesha kwamba mwanadamu aliumbwa kama nafsi mwenye maadili na uhuru wa kuchagua. Huduma ya mwanadamu haikulazimishwa; anaweza kutii au asitii. Uamuzi ulikuwa wake.” (SDA BC 1:225). Kwa bahati mbaya, mwanadamu alichagua kutotii amri bayana kutoka kwa BWANA (kama tutakavyoona katika sura inayofuata), Hawa, aliugusa Mti huo, akala matunda yake, Dhambi ikaingia, na kilichofuata ni kutengwa na Mungu, mateso ya mwanadamu, huzuni, na kifo—mauti ya milele (ikiwa dhambi isipofanyiwa toba). Lakini Mungu asifiwe kwamba Kristo aliingilia kati (Gal 4:4-5; Yn 3:16; 19:28-30). Hata hivyo, ilikuwepo ahadi iliyodokezwa katika Mwanzo 3:15 kwamba, kama mwanadamu angetubu na kuendelea katika njia ya utii, angeishi milele. Mungu asifiwe kwamba Kristo alituokoa kutokana kwenye hukumu ya kifo na kutengwa na Mungu milele. “Bali Mungu aonyesha pendo Lake Yeye Mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi” (Rum. 5:8).

Mpendwa, tunapokuja kwenye Wasaa wa Maombi leo, hebu tukumbushwe kwamba ukiukwaji wowote wa Sheria au Maagizo ya Mungu utaleta uharibifu mkubwa. Biblia inasema, “roho itendayo dhambi itakufa hakika” (Eze. 18:20). Kutomtii Mungu ni dhambi, na mshahara wa dhambi ni mauti (Rum 6:23). Usijidanganye vyovyote vile, uasi wowote wa Sheria ya Mungu utaleta matokeo ya aina fulani (ya papo hapo na ya kudumu), hata kifo. Tutubu dhambi zetu na tumtii BWANA sasa. Kwa muhtasari, sura hii inatualika — 1. Tuishike Sabato takatifu; 2. Tutii amri za Mungu; 3. Tufanye upya Nadhiri zetu za Ndoa; 4. Tuweke wakfu maisha yetu kwa Yesu; 5. Tumwombe Mungu abariki nyumba zetu. Je tuko tayari kufanya mambo haya?

Maadili ya Kukuza: Sala, Toba, Utii, Usahimishaji, Kufurahia pumziko la Mungu (Isa. 58:13; Ebr. 4:9).

Dhambi za Kuepuka/Kuungama: Tazama kipengele (1-BSG-2S) Mwongozo wa Kujifunza.

Jambo Fulani la Kumshukuru Mungu: Zawadi ya Ndoa & Familia; Baraka wa Sabato.

Watu wa Kuombewa:

  • Wanandoa Wote – Kupendana; Kujaliana, kutendeana fadhila, kuheshimiana kwa ubora zaidi (Filp. 2:3-4).
  • Kwa waume wote — kuwapenda wake zao, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake (Efe. 5:25).
  • Wadanganyifu/Wenzi Wasio Waaminifu—Kutubu na kukumbuka kwamba Siku moja, Mungu atafichua mambo yaliyofichwa ya giza na kuyafunua mashauri ya mioyo.” (1 Kor. 4:5). Waombee watubu na kuheshimu viapo vyao vya ndoa.
  • Waombee Watoto -Wawatii Wazazi wao.
  • Waombee Watu Wote – Wamtii Mungu kwa kuitakasa Siku ya Sabato.
  • Uongofu wa Kuigiza -Wanaoficha mienendo yao mibaya kwa sababu wanataka kudumisha majina yao katika rekodi ya kanisa; huku nyumbani wao ni ‘mbwa-mwitu,’ wasiomtii Mungu kwa matendo, mawazo, na mwenendo wao.

Masuala ya Kuombea:

  • Utii kwa Mungu katika mambo yote, pamoja na Amri ya Sabato.
  • Uongofu wa kweli wa wazazi/watoto walio na hatia ya chuki, vurugu nyumbani.
  • Uvumilivu & Msamaha: Kusuluhisha tofauti kati ya wenzi wa maisha, (siyo kutalakiana).
  • Neema & Ujasiri: Kumhudumia mwenzi wa maisha ambaye ni mgonjwa, mlemavu, au aliyegundulika kuwa na ugonjwa wa kufisha.
  • Uaminifu Katika Ndoa: kutendea mwenzi mwingine kwa upendo na heshima, bila kudhulumiwa wala kunyanyaswa kabisa.
  • Onyo: Wokovu wa mume unaweza kuwa hatarini ikiwa hawatafanya hivi. “Vivyo hivyo ninyi waume wapeni heshima wake zenu. Mtendee mkeo kwa busara mnapoishi pamoja. Anaweza kuwa dhaifu kuliko wewe, lakini yeye ni mshirika wako sawia katika zawadi ya Mungu ya maisha mapya. Mtendee inavyopaswa ili maombi yako yasizuiliwe.” (1 Petro 3:7, NLT).
  • Ombea imani na nguvu za kusimama imara kwa ajili ya Yesu, na kuwa imara kwa ajili ya kweli za Neno la Mungu, bila kujali matokeo yaweza kuwa nini, katika siku hizi za mwisho, hasa zaidi, kwa ajili ya kushika Sabato (cf. Ufu. 12:17).

Ahadi ya Leo: “Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.” (Ufunuo 14:12)


 

1-BSG-2Z: OMBI LA KUHITIMISHA.

Ombi la Kuhitimisha/Mwanzo 2 (1-BSG-2Z)/ Je, kuna hitaji lolote ninaloweza kuomba/kuwasilisha katika sura hii? Ndiyo.

Sala: Baba, tunakushukuru tena kwa neno Lako katika sura hii. Tunakushukuru kwa zawadi ya uzima, kwa nafasi nyingine ya kusikia Injili na kufanya mabadiliko muhimu katika maisha yetu. Tunakushukuru kwa tabia Yako isiyobadilika; kwa ahadi za zawadi; kwa ajili ya kukidhi mahitaji yetu ya kila siku.

Baba, tunakushukuru kwa zawadi ya Ndoa na Familia (Mwa 2:15-25). Familia nyingi zinasambaratika katika siku hizi za mwisho. Ibilisi ameanzisha vita katika nyumba nyingi, ikiwa ni pamoja na familia za Kikristo: ukatili unaongezeka; watoto hawawatii wazazi wao (2 Tim. 3:2); waume & wake huendelea kupigana, wakati fulani huishia kutalikiana; Wengi hawana uaminifu kwa wenzi wao; Watoto wengi hawawatii wazazi, ni wenye kiburi, watukanaji, wasio na shukrani, wasio watakatifu, wasio na upendo, wasiosamehe, wasingiziaji, wasio na kiasi, wasaliti … na orodha inaendelea na kuendelea. Utusamehe (kwa pamoja) BWANA mpendwa, na Roho Wako atusadikishe dhambi hizi.

Tusaidie kutubu na tuanze upya mchakato wa kuakisi “sura Yako” (Mwa 1:26-28) katika miili yetu, katika mienendo yetu, katika familia zetu, katika jumuia zetu. Hebu Roho Wako azibadilishe nyumba zetu ziwe “mbingu ndogo” – mahali ambapo Roho wa Mungu atakaa. Mahali ambapo Madhabahu ya Sala na Ibada itawekwa. Mahali ambapo watu kutoka mbali na karibu watakuja kuona na kujifunza upendo, neema na huruma ya Yako (cf. 2 Wafalme 20:15; Isa. 39:1-8). Mahali ambapo Malaika watakatifu watapanda na kushuka; lakini muhimu zaidi, mahali patakapoitwa kwa Jina Lako!

Naomba kwa dhati kwa ajili ya kila Baba, kila Mama: wajue kwamba kazi yao kuu ni kukuwakilisha vyema katika familia zao – kuwafundisha watoto wao — “kumlea mtoto katika njia impasayo” (Mit. 22:6), na kuwafundisha katika njia za BWANA (Kum. 4:9; 6:7; 11:19; Efe. 6:4; Kol 3:16).

Ninawaombea waume kuwapenda wake zao, “kama Kristo alivyolipenda kanisa” (Efe. 5:25-26); Vivyo hivyo na wake zao wawastahi waume zao, na kuwatii na kujisalimisha kwa waume zao (1 Pet 3:1). Tusaidie BWANA mpendwa tutubu ili kuwe na Uamsho na Matengenezo katika kila familia ya Kikristo; kwa maana hakuwezi kuwa na “kanisa mahalia” ikiwa washiriki wa kanisa (familia) wamesambaratika, na jina Lako likachafuliwa.

Ututakase, BWANA mpendwa. Katika sura hii, Unatuita ili “Tuikumbuke siku ya Sabato na kuitakasa!” (Kut. 20:8)—kwa sababu Siku ya Saba, Ulimaliza kazi Yako, ukapumzika; Ulibariki Siku ya Saba na kuitakasa (Mwa 2:2-3). Wengi wetu tuna hatia ya kuvunja amri hii. Labda tunajua kuihusu lakini hatuitii jinsi tunavyopaswa kuitii. Wapo wanaoivunja amri hii bila kujua (kwa kufuata mapokeo ya wanadamu). Wao pia uwasaidie ili waifikilie ile kweli. Utusamehe BWANA mpendwa na utukumbushe baraka nyingi ulizoweka kwa ajili ya wale watakaotii Amri Yako, ikiwa ni pamoja na Sabato (Isa. 56:2-9; 58:13-14; Eze. 20:20; Isa 66:22-23; Ebr. 4:9; Ufu. 1:3: 14:12).

Ututakase, BWANA mpendwa sawasawa na fadhili Zako, sawasawa na Neno Lako… kwamba hutaacha kutusafisha (tukikuruhusu) mpaka utakapokuwa umetukamilishwa – na kutufanya kuwa “watakatifu,” bila doa wala kunyanzi na bila lawama (Efe. 5:26-27) – hata Siku ya Bwana Yesu (2 Kor. 1:14). Tunakushukuru Baba, na tunatazamia kwa hamu “Tumaini Tukufu Lenye Baraka,” tutakapomwona Yesu uso kwa uso, wakati ambapo mambo yote yatafanywa kuwa “mapya” tena (Ufu. 21:1-4). Utujalie furaha yetu, tunasihi.

Tunakushukuru BWANA, nasi tunaomba mambo haya, tukiamini na kutumaini, katika Jina, Jina lenye nguvu zaidi, hata Jina takatifu la Yesu Kristo, Amina.


 

Wimbo wa Tafakari: Nilipotoka Kabisa (NK 118)
(I’ve Wandered Far Away)

1. Nilipotoka Kabisa, Sasa Narudi
Nikakawia Dhambini, Bwana Narudi.

Narudi Nyumbani: Daima Kwako.
Kwa Upendo Nipokee: Naja Nyumbani.

2. Nikasusurika Sana, Sasa Narudi
Mwenye Uchungu Natubu, Bwana Narudi.

3. Nimechoka Maovuni, Sasa Narudi;
Pendo Lako Lanivuta, Bwana Narudi.

4. Ndilo Tumaini Langu, Sasa Narudi;

 

Comments